
Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. MATENDO YA MITUME 17:11 BIBLIA
Kuna vitu vingi ambavyo hushawishi fikra zetu na matamanio yetu ni mojawapo. Nimegundua kwamba ninapotamani kitu kwa nguvu, ni rahisi kufikiri Mungu ananiambia nikichukue. Kwa sababu hii, lazima tuchunguze iwapo tunachoongozwa kufanya kinalingana na Neno la Mungu. Mara nyingi hutuongoza kwa matamanio, lakini tunataka kuhakikisha ya kwamba sio tu matamanio ya mwili.
Wazo lolote, la kuchochea, au fikra inayokuja kwetu inahitaji kulinganishwa na ukweli wa Maandiko. Biblia huandikwa kama barua ya kibinafsi kwa kila mmoja wetu. Mungu huongea nasi, hutimiza mahitaji yetu, na kupitia kwa Neno lake, hutuelekeza vile tunavyofaa kwenda. Kwa hivyo tunapofikiri tumesikia neno kutoka kwa Mungu, tunaweza kuchunguza ili tuone iwapo linalingana na Andiko na kushukuru kwamba tunaishi kwa Neno la hakika la Mungu.
Sala ya Shukrani
Baba, ninashukuru kwa ukweli wa Neno lako. Ninapohisi kichocheo katika roho yangu, ninashukuru kwamba ninaweza kuhakikisha kwamba kinalingana na Andiko. Leo, nitasikiza sauti yako na kuishi kulingana na kile unachoniambia na kile ulichoandika katika Neno lako.