Fanya Tu

Fanya Tu

Akasema, njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. MATHAYO 14:29

Kukosa uamuzi huharibu wakati mwingi, na wakati ni wa thamani sana kuharibu. Iwapo utakuwa mtu mwenye ujasiri na uwezo wa kuamua, utakamilisha mengi bila kutia bidii sana.

Hakuna mtu anayejifunza kusikia kutoka kwa Mungu bila kufanya makosa. Usiwe na wasiwasi sana kuhusu makosa. Usijikazie mambo sana. Wewe ni mwanadamu usiye mtimilifu mwenye uwezo wa kukosea, lakini unaweza kufurahia kwa shukrani kwa sababu unamtumikia Mungu mtimilifu asiyekosea.

Jifunze kutokana na makosa yako, rekebisha yale unayoweza kurekebisha na umtumainie Mungu kwa uongozi na ulinzi wake. Iwapo unahisi kuwa Mungu anakuchochea kupeana kitu, saidia mtu au fanya mabadiliko katika maisha yako, fanya! Chukua hatua na upande mbegu za utiifu. Ukihisi kuwa unaongozwa na Mungu, tembea kwa imani badala ya kukwama katika shaka na hofu.


Sala ya Shukrani

Baba, ninashukuru kuwa ninaweza kukuamini utanisaidia kujifunza kutokana na makosa yangu. Sihitaji kuwa na wasiwasi au kuogopa kuwa nitafanya uamuzi mbaya, kwa sababu ninajua uko nami. Asante kwamba utaniongoza na kunielekeza—hata kupitia kwa makosa yangu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon