Fanya Uwezayo na Uache Mungu Afanye Yaliyobaki

Fanya Uwezayo na Uache Mungu Afanye Yaliyobaki

Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yoyote niliyo nayo. —WAFILIPI 4:11

Huwa tunafanya kazi vizuri tunapokuwa na nia tulivu, yenye kiasi. Nia yetu ikiwa tulivu, huwa haina hofu, wasiwasi au kuteseka. Nia yetu ikiwa na kiasi vizuri, tunaweza kutazama hali na kuamua tutakachofanya au kukosa kufanya kuihusu.

Mahali ambapo wengi wetu huingia mashakani ni wakati ambao tunatoka kwenye kiasi. Inawezekana tukaenda katika hali tuli ambapo tunakosa kufanya chochote, tukimtarajia Mungu kutufanyia kila kitu, au tunashughulika kupita kiasi, tukifanya mambo katika mwili wakati mwingi. Kadri tunavyomkaribia Mungu, ndivyo tutakavyokuwa na kiasi vizuri. Tunaweza kukabiliana na hali yoyote ya maisha na kusema, “Nitafanya kile Mungu ananiongoza kufanya, lakini ninamtumainia kufanya yaliyobaki.”

Ni jambo lisilo na maana kuendelea kufanya vitu ambavyo havifanyi kazi. Mngoje Mungu na uwe mtiifu kwake, na upate kujua kwamba wakati wake ndio mtimilifu katika maisha yako. Hata kama Mungu anaonekana kwamba hafanyi lolote kuhusu hali yako, usitie hofu. Mradi tu unamtumainia Mungu, anafanya kazi, na utaona matokeo hivi karibuni.


Mara tukishafanya kile Mungu ametwambia tufanye, tunaweza kumtumainia kwa ajili ya mengine.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon