Hakikisho la Uwepo wa Mungu katika Maisha Yako

Hakikisho la Uwepo wa Mungu katika Maisha Yako

Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani. —WARUMI 1:17

Miaka mingi iliyopita, nilipokuwa nikijifunza kuhusu hakikisho na kujaribu kuishi maisha ya hakikisho, nilikuwa na wasiwasi kuhusu kufanya makosa au “kumkosa” Mungu. Ninakumbuka aliunenea moyo wangu waziwazi, akisema, “Joyce, usijali kuhusu hilo. Ukinikosa, nitakupata.” Hili hakikisho lilinisaidia kuishi maisha yangu kwa imani na tumaini badala ya hofu.

Ninapozungumza kuhusu imani, huwa mara nyingi ninatumia neno hakika, kwa sababu imani ni nia ya hakika kamilifu ndani ya Mungu. Ni hakikisho ambalo hutuleta katika utulivu wa Mungu.

Ninaamini kadri tunavyomkaribia Mungu, ndivyo tunavyozidi kuwa na hakikisho. Sio kuwa na hakika ndani yetu, lakini hakika ya wema wake na uwepo wake katika maisha yetu. Tunaweza kuwa na hakika tukiomba, hakika katika mahusiano yetu, hakika tunapofanya maamuzi, na hakika tunapofanya wajibu wetu wa kila siku.

Leo, ninawahimiza kuchukua msimamo wa ujasiri na kusema: “Nitaishi katika hakika kamilifu katika uhusiano wangu na Mungu. Ninaamini ataniongoza. Ninaamini ninaweza kufanya uamuzi mzuri. Ninaamini maombi yangu yana nguvu. Ninaamini Mungu ananipenda na ana mpango mzuri juu ya maisha yangu.”


Hauna lazima ya “kuhisi” hakika ili “uwe” na hakika!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon