Hakuna Kujifanya Tena

Hakuna Kujifanya Tena

Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo. — WAEFESO 2:10

Kwa miaka mingi nilikuwa nimetaabika na kukosa furaha. Ihali, kama watu wengine, nilijifanya kuwa kila kitu kilikuwa sawa. Sasa wanadamu hujifanya kwa manufaa ya watu wengine, bila kutaka wajue kuhusu taabu zetu, na pia tunajifanya kwa niaba yetu ili tusikabiliane na kushughulikia matatizo magumu.

Pengine haya yanaeleza juu yako. Huenda unajua vile ilivyo kuwa mtu mmoja ndani na mwingine nje. Nilijifanya kuwa mkakamavu katika maisha yangu na kwa njia nyingine nilikuwa. Bado, nilikuwa na fikra za chini kujihusu na ukakamavu niliokuwa nao haukutokana na mtu yule nilikuwa ndani ya Kristo. Ulitokana na kukubalika na watu wengine, kwa jinsi nilivyoonekana, mambo niliyokamilisha, na mambo mengine ya juujuu. Ungaliondoa mambo ya juu juu ya muda, ningaliogopa sana.

Siku ilifika nikatambua kwamba ilibidi nikabiliane na ukweli na kuacha kujifanya. Tunapojifungua kwa kweli na kuacha Mungu afanye kazi katika maisha yetu, tunaweza kuacha kujifanya kuwa kitu kisicho. Tunaweza kuwa wenye furaha na uhuru, tukifurahia mtu ambaye Mungu alifanya kila mmoja wetu kuwa.


Kwa kweli huwa hatujawahi kuwa huru hadi tuweze kuishi bila kujifanya na kuridhika na vile tulivyo!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon