Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote. Warumi 12:18
Somo muhimu nililojifunza ni “kuinama ili nisivunjike.” Biblia inasema kwa Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi na [watu, vitu]. Na, ikiwa inawezekana, kama inakutegemea, uishi kwa amani na kila mtu (Warumi 12:16, 18).
Kabla ya kulifanya Neno la Mungu kuwa kipaumbele katika maisha yangu na kuamua kuishi maisha ya kutii, nilikuwa na njia yangu mwenyewe. Sikuweza kubadilika; nilitaka kila mtu mwingine awe kama mimi. Bila shaka, hiyo ilisababisha ugomvi zaidi na msongo wa akili.
Sasa nimejifunza kuinama. Si rahisi sana kwa mwili kuacha kufanya mambo tofauti kuliko nilivyopanga, lakini ni rahisi kuliko kuwa na hasira na kusikitika.
Ikiwa unataka kuwa na amani katika mahusiano yako, unahitaji kuwa na hamu ya kubadilika. Kusukuma kwa njia yako mwenyewe wakati wote utakuumiza tu na kuwaumiza wale walio karibu nawe. Lakini unapochukua moyoni ushauri wa Paulo kuwa na amani na kila mtu, Roho Mtakatifu atajaza uhusiano wako na furaha na amani
OMBI LA KUANZA SIKU
Roho Mtakatifu, nisaidie kuinama ili nisivunjike. Mimi nataka amani yako katika mahusiano yangu, kwa hiyo ninachagua kubadili leo.