Ishi Maisha ya Roho

Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa Roho wa Kristo, huyo si wake (Warumi 8:9)

Tumeitwa kutembea katika Roho, au vile andiko la leo linasema, “kuishi maisha ya Roho.” Kufanya uamuzi kufanya hivi ndilo jambo la kwanza, lakini ninaweza kukuambia kutokana na Neno la Mungu na kutokana uzoefu kwamba huchukua zaidi ya uamuzi; inachukua kazi ya ndani ya Roho Mtakatifu katika maisha yetu. Hutufanyia “upasuaji” kwa Neno la Mungu,   ambalo huchoma hata kuzigawanya nafsi na roho (Waebrania 4:12). Hutumia pia hali kutufundisha kuwa imara na kutembea katika upendo kila wakati.

Hivi vitu ambavyo tumeitwa kufanya sio vitu tu tunavyopewa; lazima vifanyishwe kazi ndani yetu. Kama tu vile lazima hamira ifanye kazi ndani ya kinyunya- hivyo ndivyo Kristo anafanyishwa kazi ndani yetu.

Katika Wafilipi 2:12, Mtume Paulo anatufundisha “tuutimize” wokovu wetu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. Hiyo ina maana kwamba tunafaa kushirikiana na Roho Mtakatifu anapoanza ndani yetu kazi kusulubiwa au “kufa nafsi.” Paulo alisema, “ninakufa kila siku.” (1 Wakorintho 15:31). Kwa maneno mengine, alikuwa anasema kwamba alikuwa “akifa mwili.” Hakuwa anazungumza kuhusu kifo cha kimwili, lakini kifo cha hiari na njia zake.

Iwapo tunataka kweli kuishi maisha ya Roho, lazima tuue hiari na njia zetu na kuchagua mapenzi ya Mungu. Tunaweza kumtegemea Mungu kutuongoza, na tunataka aweze kututegemea kumtii.

NENO LA MUNGU KWAKO LEO:

Ukifa nafsi, utaweza kuhudumu maisha kwa wengine.  

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon