Kubariki Walio Karibu Nawe

Kubariki Walio Karibu Nawe

. . .Na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, ni heri kutoa kuliko kupokea. MATENDO 20:35

Ni mapenzi ya Mungu kuwa tutoe shukrani wakati wote na kwa kila kitu (tazama 1 Wathesalonike 5:18). Ili kutoa shukrani kikamilifu lazima ionyeshwe kwa matendo. Tunaweza kusema kwamba tunashukuru, lakini tunaonyesha shukrani? Tunasema “asante,” lakini kuna njia zingine za kuonyesha shukrani, na mojawapo ni kubariki wengine.

Kutoa ili kusaidia wengine ni mojawapo ya njia ambazo tunaweza kuendeleza mzunguko wa baraka katika maisha yetu. Mungu hutupatia na tunaonyesha shukrani kwa kumpa mtu mwingine, halafu anatubariki zaidi ili tufanye hivyo tena. Tunachowapatia watu wengine kama matokeo ya utiifu kwa Mungu hakipotei. Kinaondoka katika mikono yetu kwa muda mfupi, lakini hakitoki katika maisha yetu. Tunakitoa, Mungu anakitumia kubariki mtu mwingine, na tunabarikiwa pia.


Sala ya Shukrani

Asante, Baba, kwamba wewe hunibariki ili niwe baraka kwa wengine. Nisaidie kutafuta njia ya kuwapa wale walio karibu nami leo. Ninashukuru kwa wema wako, na ninataka nionyeshe shukrani hiyo kupitia kwa ukarimu wangu kwa wengine.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon