Kujitayarisha kwa ajili ya Mazuri

Kujitayarisha kwa ajili ya Mazuri

Mpigieni Bwana vigelegele, enyi wenye haki, kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo. — ZABURI 33:1

Vile tunavyokaribia kila siku mpya na kila hali mpya huleta tofauti kubwa. Tukiamua mapema kwamba hatutakuwa na furaha wala amani hadi tupate kabisa tunachotaka, basi tutakuwa na amani kwa nadra.

Nimesikia watu wakisema vitu kama, “Ikinyesha kesho sitakuwa na furaha,” au “Nisipopata kazi hiyo, nitasikitika sana.” Tukiwaza mawazo kama hayo, tunajitayarisha kupoteza amani na furaha hata kabla tuwe na shida.

Badala ya kujitayarisha kusikitika, tunaweza kujitayarisha kuwa na amani. Tunaweza kufikiri na kusema vitu kama, “Kwa kweli ninatumai hali ya anga itakuwa nzuri kesho, na ninatumai nitapata hii kazi mpya. Lakini furaha yangu hutoka kwa uhusiano wangu na Yesu, kwa hivyo ninachagua kuwa na furaha na kuwa na utulivu ndani ya moyo wangu hata nikikabiliana na kitu chochote kesho. Hata kunyeshe au kuwake jua, hata nipate kazi hiyo au nisiipate, ninachagua furaha ya Bwana!”
Vile tunavyokabili maisha yetu huleta tofauti katika ubora wa maisha tunayoweza kuwa nayo. Tunaposhindwa kuimarisha maisha, wacha tukumbuke kwamba tunaweza kuimarisha jinsi tunavyokabiliana nayo.


Amua kwamba utakuwa na furaha mambo yakienda unavyotaka leo…na yasipoenda hivyo.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon