Kujitolea katika ndoa

Kujitolea katika ndoa

 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 1 Wakorintho 13:1

 Mwanzoni mwa ndoa yetu, ilibidi Mungu anifundishe kwamba kweli kumpenda Dave ilimaanisha kuwa wakati mwingine ningehitajika kujitolea. Hadi mpaka hapo, nilitaka njia yangu tu na nilikuwa kama shaba la kelele lililoelezwa katika 1 Wakorintho 13: 1.

Upendo ni ishara ya juu kuhusu ukomavu. Mara nyingi inahitaji zawadi ya dhabihu. Ikiwa upendo hauhitaji aina ya dhabihu kwa upande wetu, labda hatupendi mtu mwingine kabisa. Ikiwa hakuna dhabihu katika matendo yetu, tunaweza kujibu kwa kitu kizuri ambacho walitufanyia, au tu kujifanya kuwa wema ili kupata udhibiti juu yao.

Ni muhimu kuelewa kwamba upendo wa kweli unatoa wenyewe. Kwa hivyo maamuzi yako lazima daima yatilie maslahi ya mwenzako moyoni. Unapofanya hivyo, unajitoa mwenyewe.

Tamaa ya Mungu ni kwa waume na wake kupendana kwa kujitolea na bila kujali. Hii inamaanisha huwezi kupata njia yako wakati wote. Lakini habari njema ni, wakati mume na mke wanapoachilia tamaa zao za ubinafsi, watakuwa na ndoa ya ushindi!

 OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, nataka kutembea katika upendo wa kweli katika ndoa yangu. Ninafanya uamuzi leo kutoshinikiza kila wakati kwa njia yangu mwenyewe, lakini kuwa tayari kujitolea kwa mwenzangu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon