Kuongozwa na Roho Mtakatifu

Bali ninyi wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu. — YUDA 20

Kama tu Waefeso 6:18 inavyotuambia kuwa tunafaa kuomba wakati wote kwa aina zote za maombi, tunaambiwa na Yuda pia kwamba maombi yetu yawe “katika Roho Mtakatifu.” Mtume Paulo anatuambia katika Warumi 8:26 kwamba tunapokosa kujua kuomba, Roho Mtakatifu anajua vile atatuombea katika udhaifu wetu.

Ni Roho Mtakatifu peke yake ndani yetu ambaye hutuchochea na kutungoza kuomba. Badala ya kuchelewa, tunaweza kujifunza kukubali uongozi wa Roho punde tunapouhisi. Hiyo ni sehemu mojawapo ya kujifunza kuomba aina zote za maombi wakati wote, popote tulipo na tunachofanya chochote.

Wito wetu unaweza kuwa kama wimbo wa kiroho wa kale, “Kila wakati nikisikia Roho akiwepo moyoni mwangu, nitaomba.” Tunapojua kwamba tunaweza kuomba wakati wowote na mahali popote, hatutahisi kwamba tuko mbali na Mungu, na hatutahisi kwamba lazima tungoje ule wakati mzuri au mahali ili tuombe.

Tunapoongozwa na Roho Mtakatifu, tunaweza kujua kwamba maombi yetu yanafika katika kiti cha enzi cha Mungu na yatajibiwa.


Mwombe Roho Mtakatifu ahusike katika kila unalofanya. Yeye ni Msaidizi, na anakungoja wewe uombe.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon