
Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala wasikate tamaa. LUKA 18:1
Maombi yanaweza kuwa kama kupumua—ya kila mara, rahisi, utu wa pili—na tunaweza kuomba maishani kama sehemu ya tunavyoishi. Kwa kweli vile maisha ya kimwili yanavyoendelezwa kwa kupumua, maisha yetu ya kiroho yanafaa kudumishwa kwa maombi.
Tunaweza kuomba kwa sauti ya juu au sauti ya chini. Tunaweza kuomba tunapokuwa tumekaa, kusimama, au kulala sakafuni. Tunaweza kuomba tunapokuwa safarini au tunapokuwa tumetulia. Tunaweza kuomba tunaponunua vitu, tunapongoja miadi, tunaposhiriki katika mkutano wa biashara, tunapofanya kazi za nyumbani, tunapoendesha gari au tunapooga. Hizi ni nyakati nzuri za kutoa maombi ya shukrani. Tunaweza kuomba vitu kama, “Asante Bwana, kwa vitu vyote unavyofanya,” au, “Sifu Mungu, ninajua uko nami katika hali hii.” Maombi ni kuongea tu na Mungu na kueleza moyo wako kwake, na hilo linaweza kufanyika wakati wowote, popote.
Sala ya Shukrani
Baba, asante kwa kipaji cha maombi. Haijalishi siku yangu inavyoonekana, ninashukuru kwamba ninaweza kuchukua wakati kuomba katika kila hali, nikiwa na hakika kwamba unasikia na kunijibu.