
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake ni za milele. ZABURI 106:1
Mungu ni mwema kwetu kila wakati, mwaminifu kwetu kila wakati, na kufanya kazi kwa bidii kila wakati katika maisha yetu. Kila wakati anatufanyia kitu kwa maslahi yetu, kwa hivyo tunahitaji kuitika kwa kumjuza kwamba tunafurahia wema wake mwingi.
Kwa mfano, “Bwana, asante kwa usiku wa usingizi mzuri,” au “Mungu, ninakushukuru kuwa nilipomtembelea daktari wa meno, sikuhisi uchungu sana vile nilivyofikiri,” au “Baba, asante kwa kunisaidia kufanya uamuzi mzuri leo,” au Bwana, asante kwa kuendelea kunihimiza.”
Tunaweza kumshukuru Mungu kwa kimya katika mioyo yetu, na tunaweza kumshukuru kwa sauti pia kwa sababu hilo hutusaidia kukaa tukitambua na kufahamu upendo wa Mungu, ambao anatuonyesha kupitia kwa wema wake kwetu.
Sala ya Shukrani
Ninakushukuru, Baba, kwa uaminifu wako kwangu kila wakati. Hata wakati sikioni, unafanya kazi kwa niaba yangu kwa sababu unanipenda na una mpango mkubwa juu ya maisha yangu. Asante kwa njia zote ambazo huwa unaonyesha upendo huo kila siku.