Nia za kimungu

Nia za kimungu

Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu; Zaburi 139:23

Miaka iliyopita tulipokuwa tunashindwa kifedha, nilikuwa nimechoka kwa kuamini kwa mafanikio na nikavunjika mbele ya Bwana.  Nililia kuyahusu kwa muda na kisha, kwa neema ya Mungu, nilifanya uamuzi na kusema: “Mungu, nitaendelea kutoa zaka na kutoa sadaka mpaka siku nitakapokufa, ikiwa chochote kitakuja kutokana nayo au la ! ”

Naamini kwa moyo wangu wote huu ulikuwa mtihani kwangu kuona ni kwa nini nilikuwa ninatoa. Bwana alitaka kufunua ikiwa nilikuwa na maadili ya kimungu. Ikiwa ningekuwa “natoa tu kupata,” ningeweza kuwa na ubinafsi tu kutaka kupewa kitu kutoka kwa Mungu.

Kumekuwa na mafundisho mengi na mahubiri ambayo yanasema, “Fanya hili na utapata hilo.” Lakini vipi kuwa na moyo safi unaosema, “Ninataka kufanya jambo lililo sawa kwa sababu ni sawa na linamtukuza Mungu”?

Ninakuhimiza kwa uaminifu kuchunguza nia zako leo na uhakikishe kuwa sio ubinafsi. Fanya uamuzi kujitoa kwa moyo wote kumtumikia Mungu kwa sababu sahihi.

OMBI LA KUANZA SIKU

Roho Mtakatifu, chunguza moyo wangu na uonyeshe nia na maadili yangu ya kweli leo. Ikiwa sio ya kiungu katika eneo lolote, nionyeshe na unisaidie kubadili.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon