Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo. WAGALATIA 1:10
Ushawahi kuhisi kwamba hukuweza kuwa kila kitu ambacho kila mtu alitaka uwe? Ushawahi kujua kwamba chini zaidi ndani kwamba kweli ulihitaji kusema “la” kwa watu wengi—lakini hofu ya kutowapendeza ikafanya mdomo wako useme, “Nitajaribu,” huku moyo wako ukipiga ukelele, “Siwezi kufanya!”?
Wakati mwingine watu wasiokuwa na usalama husema “ndiyo.” Wale ambao hufanikiwa kuwa wao, huwa hawaruhusu wengine kuwadhibiti. Huongozwa na moyo jasiri unaojua kwamba Mungu anawapenda, sio na hofu ya kutowapendeza wengine au kukataliwa nao.
Hatufai kuwakasirikia watu kwa sababu wanaweka madai juu yetu, kwa sababu kwa kweli ni wajibu wetu kuendesha maisha yetu. Shukuru kwamba, tunaweza kupata usalama ndani ya Kristo na tuwe na ujasiri wa kutosha kusema “la” kwa watu tukijua ndicho kitu sawa cha kufanya.
Sala ya Shukrani
Ninapokuwa katika hali ambapo, Baba, ninajaribiwa kujisalimisha kupita mipaka juu ya kitu au mtu hata kama sina amani kukihusu au kumhusu, nisaidie kuwa na usalama wa kutosha ili kusema “la”. Ninakushukuru kwamba usalama wangu unapatikana ndani yako, sio katika kupendeza wengine.