Ufahamu wa Upendo wa Mungu

Ufahamu wa Upendo wa Mungu

Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. —1 YOHANA 4:16

Katika 1 Yohana 4:16, Biblia inatuagiza “kuelewa, kutambua” na “kufahamu” upendo Mungu alio nao juu yetu. Kuwa katika uhusiano wa karibu na wa kibinafsi na Mungu ni kufahamu upendo wake wakati wote na kuendelea kushangazwa na ukweli kwamba anatuonyesha upendo wake juu yetu hata kama hatuustahili.

Jambo moja ambalo nitakuhimiza kufanya ni kuweka kitabu cha ukumbusho, kitabu ambacho unaandika vitu muhimu ambavyo Mungu amekufanyia. Ukianza kuchunguza na kuandika kuhusu wema wa Mungu kwa njia hii, utashangaa vile mara nyingi upendo wa Mungu hudhihirika kwa njia tekelezi (ndogo na kubwa) katika maisha yako.

Upendo wa Mungu unaweza kubadilisha maisha yako ukiuruhusu. Una nguvu ya kuponya majeraha ya hisia. Upendo wake hukutia nguvu za kuchuchumilia mbele katika nyakati ngumu, na kulegeza moyo wako, huku ukikuwezesha kuonyesha upendo zaidi kwa wengine. Unaweza kufikiria kitu kingine kilicho bora cha “kufahamu” na kujua kuliko huu upendo mkuu?


Pengine kitu kizuri unachoweza kufanya leo ni kuchunguza tu upendo wa Mungu, kuutambua na kuusherehekea kwa shukrani.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon