Uzoefu Wa Maombi

Uzoefu wa Maombi

Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali, saa tisa… —Matendo Ya Mitume 3:1

Watu wengi huhisi kuhukumika kwa mbali kuhusu maisha yao ya maombi kwa sababu wanajilinganisha na wengine. Mungu ni Mungu mbunifu na anataka kila mtu kuwa na maisha yake binafsi ya maombi. Maisha yako ya maombi hayapaswi kuwa tu kama ya mtu mwingine.

Ndiyo, kuna kanuni zilizothibitishwa za maombi ambazo unaweza kufuata. Vile tunavyoona katika Matendo ya Mitume 3:1, mitume wa awali walitenga kando masaa fulani ya siku ambapo walienda katika sehemu walizopanga ili kuomba. Hiyo ni nidhamu nzuri ya kibinafsi, lakini huo uwe mwanzo wa kujifunza kuomba wala siyo mwisho. Tunaweza kujifundisha kuwa na nidhamu ya kupanga ratiba ya maombi ambayo inatufaa sisi wenyewe binafsi, lakini pia tunaweza kujifunza kuomba bila kukoma. Hiyo inamaanisha kuomba kila wakati, mahali popote, kwa kila aina ya maombi. Ninapenda kusema, “Omba mchana kutwa.” Acha maombi yawe kama kupumua, kitu unachofanya kwa urahisi bila kutumia nguvu zozote.

Hatufai kusema “ngoja” nitaomba baadaye. Kila wakati unapoona hitaji au kufikiri kuhusu kitu kinachohitaji usaidizi wako, omba moja kwa moja! Maombi ni kuzungumza na Mungu, na kwa kuwa yuko kila mahali, tunaweza kuzungumza naye kila wakati.


Mungu anataka maombi yawe sehemu ya kila siku, na ya mara kwa mara ya maisha yetu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon