Uhusiano, Si Kanuni

Uhusiano, Si Kanuni

Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama… —EZEKIELI 36:26

Mara nyingi mtu akizaliwa upya, mambo ya kwanza wanayoelezwa ni: “Unahitaji kubadilisha mtindo wako wa nywele, au uvae kitofauti. Una chale inayohitaji kufinikwa. Una kipuli mahali pasipostahili.” Ukaribishaji wao katika Ukristo ni orodha ya kanuni, vitu vinavyopaswa kufanywa na visivyopaswa kufanywa kulingana na vile watu wanafikiria kwamba ni sawa au si sawa kufanya.

La kuhuzunisha ni kwamba, hakuna anayezungumza nao kuhusu mioyo yao au uhusiano wao na Mungu. Badala yake, mazungumzo yanahusu vitu ambavyo wanafaa kufanya ili wawe wamojawapo wa washiriki wa shirika fulani la kidini. Hata ingawa Mungu atatuongoza kufanya mabadiliko chanya katika maisha yetu, anatukubali kabisa jinsi tulivyo, na tunahitaji kufanya vivyo hivyo kwa Wakristo wapya. Wape muda, na Mungu atawaongoza kwa kuwapa matamanio mapya.

Yesu alikufa ili tuwe na uhusiano wa ndani, wenye kuwa na hamu, na uhusiano na Mungu. Hakufa kutupatia orodha ya kanuni. Alitupatia kitu cha ndani zaidi na kilicho bora zaidi—Alitufungulia njia ya kumfikia Mungu ili tuwe katika uhusiano wa karibu na wa kibinafsi na Baba yetu wa mbinguni.

Kadri unavyomkaribia Mungu, ndivyo anavyokubadilisha toka ndani hadi nje kwa upendo na neema.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon