Sherehekea Uhai

Sherehekea Uhai

Mwanadamu hapati jema kupita kula na kunywa, na kuiburudisha roho yake kwa mema katika kazi yake. Hayo nayo naliona ya kwamba hutoka mkononi mwa Mungu. —MHUBIRI 2:24

Inawezekana kuishi maisha kwa utulivu—kwa kupitia shughuli za kufanya kazi, kufanya na kukamilisha mambo lakini kwa kweli bila kufurahia maisha. Hili ni kweli kuhusu watu ambao hawajajifunza kukumbatia na kupenda Maisha ambayo Mungu amewapa.

Kufurahia maisha ni uamuzi, hakutegemei mazingira au hali ya furaha ya muda. Ni mwelekeo wa moyo, uamuzi wa kufurahia kila kitu, kwa sababu kila kitu—hata kidogo, vitu vinavyoonekana kutokuwa muhimu—vina nafasi katika “picha kuu” ya Mungu kwa ajili ya maisha yetu.

Furaha yetu inapatikana ndani ya Yesu, na tukifanya yote tunayofanya naye na kwa ajili yake, basi tunaweza kufurahia vyote kwa kweli. Hata kama tuna shida ambazo tunamngoja Mungu kusuluhisha, tunaweza kufurahia maisha yetu bado. Shaka na kutokuamini ni wezi wa furaha, lakini imani ya upesi kama ya mtoto huachilia furaha iliyofanya makao ndani ya roho zetu kwa sababu Roho Mtakatifu anaishi hapo. Amini Mungu kila wakati na ufurahie uwepo wake! Maisha yako ni kipawa kutoka kwake, kwa hivyo yasherehekee!

Unaweza kuchagua kusherehekea katika furaha ya Mungu na kufurahia kila siku ya maisha yako naye!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon