Endelea na ufurahie maendeleo yako

Endelea na ufurahie maendeleo yako

Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.  Zaburi 119:105

Ni kweli kwamba sisi wote tuna nafasi ya kukua na kujiboresha katika uhusiano wetu na Mungu. Nilikuwa nimekata tamaa kuhusu jinsi nilivyohitaji kwenda, na ilionekana kama nilikumbushwa kila siku, wakati mwingine kila saa. Nilikuwa na hisia ya kushindwa mara kwa mara-hisia kwamba sikuwa yule niliyehitajiwa kuwa, sikuwa natosha na nilihitaji kujitahidi zaidi. Hata hivyo, wakati nilijitahidi kwa bidii, nilishindwa tena.

Lakini sasa nimekuza mtazamo mpya: Siko ambapo ninahitaji kuwa, lakini asante Mungu kwani siko nilipokuwa mbeleni. Mimi niko sawa, na niko njiani! Sasa najua kwa moyo wangu wote kwamba Mungu hajakasirika nami kwa sababu sijafika bado. Anapendezwa kuwa ninaendelea na kuendelea na njia ambayo ameniandalia.

Ikiwa wewe na mimi “tutazidi kuendelea,” Mungu atafurahia maendeleo yetu. Ameahidi kuangaza njia mbele yetu. Hatuwezi kujua njia, na tunaweza kuanguka mara kwa mara, lakini Mungu ni mwaminifu. Anaona maendeleo yako, Yeye anajivunia kwako, na Yeye atakusaidia kukua kwenye njia sahihi!

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, siwezi kukata tamaa kuhusu mahali nilipo. Tayari umenileta umbali huu, na najua utazidi kuiangaza njia yangu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon