Usichoshwe sana kwa ajili ya shuguli nyingi

Usichoshwe sana kwa ajili ya shuguli nyingi

Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. itieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi. —Mathayo 11:28-30

Katika siku za mwanzo za kutembea kwangu na Bwana, nilikuwa na shauku kubwa na nia ya kumtumikia, hivyo nikajiandikisha kwa kila kitu ambacho kilionekana kuwa kivutio kwangu. Moja ya matokeo ya yote ni kwamba kwa haraka niligundua kile nilikuwa nimepakwa mafuta kufanya.

Kwa sababu ya maisha yangu ya shuguli nyingi, sikuwa na muda pamoja na Mungu mara kwa mara. Nilikuwa nikifanya mambo mema kwa ajili ya Mungu, lakini kwa namna fulani nikamweka kando. Matokeo yake, mara nyingi nilihisi kuchanganyikiwa kwa sababu nilikuwa nikifanya kazi za mwili.

“Matendo ya mwili” ni mambo tunayofanya bila nguvu ya Mungu kutenda kati yetu. Vitu hivyo ni vigumu, hutuchosha, na havina furaha au kutimiza. Mara nyingi ni mambo mazuri, lakini sio “Mambo ya Mungu.”Watu wanaweza kuchoshwa juu ya shughuli za kidini huku wakijitahidi kumtumikia Mungu kwa nguvu zao wenyewe. Lakini Yesu hakukufa kwa ajili yetu kuwa na shughuli zisizo na mwisho … Alikufa ili tuweze kuwa mmoja na Mungu kupitia kwake, ili tuweze

kuwa na uhusiano wa kina na Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu. Je! Unahitaji kukata kazi za kimwili leo na kwa kweli kuwa pamoja na Mungu?


Ombi La Kuanza Siku

Bwana, mimi natambua kwamba kufanya kazi njema hakuwezi kuchukua nafasi ya kukujua kweli. Nisaidie kupata pumziko langu ndani yako hata ninapoweka shughuli zisizofaa kando ili kutumia muda zaidi na Wewe.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon