Kuchagua Kuvumilia

Kuchagua Kuvumilia

Kwa sababu hiyo nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu. Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi. —2 Timotheo 1:6–7

Katika siku ngumu itasaidia kukumbushwa kuvumilia ili kutimiza mwito wa Mungu juu ya maisha yetu. Katika hizo siku unapohisi kukata tamaa, kumbuka tu kwamba Mungu amekupa nguvu za kuvumilia!

Katika andiko la leo, tunajifunza kuwa Timotheo alikuwa mhubiri mchanga ambaye alihisi kukata tamaa. Moto ambao uliwaka ndani yake wakati mmoja ulikuwa umeanza kuzima. Siku hizo kanisa lilikuwa linapitia katika mateso mengi, na Timotheo alikuwa na woga fulani. Pengine alihisi uchovu na kila kitu kilikuwa kinamsambaratikia. Alikuwa amefika mahali ambapo alihitaji kuhimizwa ili kujichochea katika imani.

Paulo alikuwa akisema, “Timotheo, huenda unahisi kukata tamaa, lakini ninakukumbusha kuhusu mwito ulio juu ya maisha yako. Kumbuka nguvu za Roho Mtakatifu zilizobadilisha maisha yako. Anakupa roho wa nguvu, upendo, nidhamu na kujidhibiti binafsi” Paulo alimhimiza Timotheo kuwa thabiti.

Tukiwa na udhabiti, tunafanya kinachostahili hata kama ni vigumu na hatuhisi vizuri. Himizika leo kwamba unaweza kufanya chochote unachohitaji. Ndani ya Kristo, unaweza yote!


Kukata tamaa ni chaguo tu la wale wanaopanga kutofaulu katika maisha.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon