Kufuata Maagizo ya Mungu

Kufuata Maagizo ya Mungu

Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako. Kwa maana nimependezwa nayo. ZABURI 119:35 BIBLIA

Ni muhimu kujua kile Neno la Mungu linasema kuhusu nafasi yake katika maisha yako, kwa sababu linathibitisha mpango wake wa uungu wa kujihusisha kindani na kila linalokuhusu wewe. Neno la Mungu linasema “Tumtambue yeye, naye atayanyosha mapito yetu (tazama Mithali 3:6). “Kumtambua Mungu” inamaanisha kujali anavyofikiri na kutaka maoni kutoka kwake.

Mithali 3:7 inasema, “Usiwe mwenye hekima machoni pako.” Kwa maneno mengine, usifikiri hata unaweza kuendesha maisha yako na kufanya kazi nzuri bila usaidizi na uelekezi wa Mungu. Lakini, shukuru Mungu, kwa kuwa huwa anatupatia maagizo yake ili tugundue vyote alivyo navyo kwa ajili yetu tunapomfuata! Tunaweza kuamini uongozi wake na kufanya anachotuambia tufanye.


Sala ya Shukrani

Baba, ninapokabiliwa na hali fulani mahali ambapo sina hakika ya kile nitakachofanya, ninaomba kwamba unipe mwelekeo dhahiri. Ninakushukuru kwamba ninaweza kukutambua na kuegemea Neno lako ili kupata mwelekeo bila kujali hali inayonikabili.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon