Kukomesha Yo-Yo za Kihisia

Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi… —Wagalatia 5:22–23

Ninakumbuka miaka ambayo nilikuwa ninachokiita “Mkristo yo-yo.” Nilikuwa juu na chini kihisia kila mara. Mume wangu Daudi alipofanya nilichopenda mimi, nilifurahi. Alipokosa kufanya nilichopenda, nilishikwa na wazimu. Nilikuwa sijajifunza namna ya kuongozwa na Roho Mtakatifu na nilikuwa nikiacha hisia zangu kudhibiti tabia zangu.

Zaidi ya kitu chochote, waaminio huniambia vile wao huhisi. “Ninahisi hakuna anayenipenda.” Ninahisi mwenzangu hanifanyii inavyofaa.” “Ninahisi kwamba sitawahi kuwa na furaha.” “Ninahisi…sihisi…” na zaidi na zaidi yanaendelea.

Mungu anataka tutambue kwamba hisia zetu hazitaisha, kwa hivyo lazima tujifunze kuzidhibiti badala ya kuziacha zitudhibiti. Tunaweza kuchagua kujizoesha kujidhibiti na kutoruhusu mwili wetu kututawala. Hakuna mmoja wetu ambaye atawahi au hata anafaa kupata kila kitu anachotaka. Aaminiye aliyekomaa kiroho anaweza kuwa mwingi wa amani na furaha hata kama hatopata anachotaka.

Tunaweza kuchagua kujiambia kwamba hatutaweza kusema kila kitu tunachotaka kusema, kula kila kitu tunachotaka kula, na kila mara kufanya kila tunachohisi tunataka kufanya. Chagua kuacha Roho Mtakatifu akusaidie kufanya kilicho sahihi bila kujali unavyohisi!


Kama Wakristo, badala ya kubanwa na vile tunavyohisi, tunaweza kulenga tunachojua kuwa ni ukweli katika Neno la Mungu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon