Kuwa kitu kimoja munamaanisha kufurahiana

Kuwa kitu kimoja munamaanisha kufurahiana

Wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 1 Petero 3:2

Unaweza kuwa na furaha ya ajabu katika ndoa yako unapoanza kufurahia. Je! Unajua Mungu hakuwaweka pamoja ili muwe na huzuni? Yeye hakuwaweka pamoja ili mpigane, mtoane makosa au mjaribu kubadilishana.

Biblia inasema hasa kwamba mwanamke amfurahie mumewe, lakini naamini maandiko haya yanatumika kwa pande mbili za ndoa. Hata hivyo, ni mara chache nimesikia mwanamke akisema, “Unajua nini? Ninafurahia sana mume wangu, “au kusikia mwanamume anasema,” Ninafurahia mke wangu. ”

Lakini katika ndoa, Mungu anataka tufurahi. Anataka wewe na mwenzako mcheke na kufurahia pamoja. Ninakubali kwamba si rahisi kila wakati. Ndoa dhahiri ina changamoto zake; lakini licha ya tofauti zenu, mwombe Mungu akuonyeshe mambo mazuri kuhusu mwenzako. Mwambie akusaidie kumwona mwenzako jinsi Yeye anamuona, kwa sababu anawapenda na alikufa kwa ajiliyao kama alivyokukufia.

Wakati una mtazamo wa Mungu kwa kila mmoja, furaha itajaza moyo wako kwa kawaida na utaweza kufurahia mwenzako.

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, nataka kumfurahia mwenzangu. Hata wakati ndoa ni ngumu, nisaidie kupata furaha na kumfurahia  kwa kumuona jinsi unavyomuona

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon