Kuona Watu vile Mungu Anavyowaona

Kuona Watu vile Mungu Anavyowaona

Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. —WAFILIPI 2:4

Tatizo kubwa leo miongoni mwa waaminio ni choyo na ubinafsi. Tusipokuwa waangalifu, tunaweza kujifikiria kiasi kwamba hatutajua furaha ya kweli ya kujisahau na kumtumikia Mungu kwa kusaidia wengine. Tunapowasaidia wengine, Mungu hutusaidia na kushughulikia mahitaji yetu. Kile tunachofanya kifanyike kwa mtu mwingine, Mungu hukifanya kifanyike kwetu.

Ni rahisi kuhukumu na kuwatoa makosa watu wengine, lakini Mungu anataka tuwapende badala yake. Anataka tuwaonyeshe rehema aliyotuonyesha. Neema hushinda juu ya hukumu kulingana na Neno la Mungu, kwa hivyo wacha tujishughulishe kuwa baraka na furaha yetu itaongezeka.

Ni vigumu kuwa mchoyo na kuwa na furaha wakati huohuo. Furaha huja tu kwa kufikia wengine na upendo wa Mungu. Kadri tunavyojifikiria wenyewe ndivyo tunavyokuwa na dhiki zaidi. Niliishi miaka mingi nikiwa sina furaha kwa sababu tu sikuwa nikimfanyia yeyote kitu. Mwishowe nilijifunza kwamba Mungu hakutuumba “kujifikia ndani” bali “kufikia nje” wengine. Unapowafikia watu nje, basi Mungu atakufikia ndani na kukutana na mahitaji yako yote.


Mwombe Mungu akuonyeshe yule unayeweza kusaidia na kubariki leo.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon