Kusafishwa kwa Moto

Bwana naye akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, ili awaongoze njia na usiku ndani ya moto mfano wa nguzo ili kuwapa nuru; wapate kusafiri mchana na usiku (Kutoka 13:21)

Katika sehemu kadhaa za maandiko, biblia inataja moto wa Mungu na vile unavyotumiwa katika maisha yetu. Iwapo tunataka mema ya Mungu, lazima tuvumilie mioto ya kusafishwa. Tuna dhahabu ndani yetu (vitu vizuri), lakini pia tuna uchafu pia unaofaa kuondolewa.

Kila mtu anataka kufurahia mambo mema kabisa ya Mungu, lakini ni wachache walio tayari kufuatwa na moto wake. Kumbuka kila wakati kwamba, moto wa Mungu unapokuja katika maisha yako, huwa amesimamia mwale. Hawezi kuachilia moto ukazima kabisa, lakini hawezi pia kuachilia ukuharibu. Huwa hauachilii kutujilia zaidi kuliko uwezo wa kuustahimili.

Katika maisha yetu yote tunapitia nyakati ambazo zinaonekana kuwa ngumu na nyakati zingine rahisi. Paulo alirejelea nyakati hizi na kusema kwamba alikuwa amejifunza kuridhika kwa yote. Aliamini kwamba hekima ya Mungu ilikuwa timilifu na kwamba vitu vyote vitatenda kazi kwa ajili ya wema wako. Tunaweza kuchagua kufanya hivyo. Kupinga moto wa Mungu hautauzuia kuwaka ndani ya maisha yetu- inafanya tu iwe vigumu kuvumilia.

Moto wa Mungu huja kuchoma vitu vyote vibaya katika maisha yetu na kuacha kilichoachwa kiking’aa kwa ajili yake. Wakati mwingine tunahisi moto huu ndani yetu tunaposoma Neno la Mungu na kuthibitishiwa eneo linalohitaji mabadiliko. Wakati mwingine, moto wa Mungu huja kupitia kwa hali zisizofurahisha ambazo Mungu hututaka kusalia tukiwa imara na kuonyesha tabia za kiungu. Wakati wowote tunapovumilia kitu kigumu kwa sababu ya utukufu wa Mungu tunaweza kuhakikishiwa kwamba tuzo yetu itakuja hatimaye.

NENO LA MUNGU KWAKO LEO: Ukipitia mambo mengi, basi hutayatoroka au hata kuyaogopa.  

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon