Kuwa Mvumilivu

Kuwa Mvumilivu

Subira na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno. —Waraka Wa Yakobo 1:4

Yakobo anatufundisha kwamba tunaweza kufurahia tunapojipata tumehusika katika hali ngumu, tukijua kwamba Mungu anajaribu imani yetu ili kuleta uvumilivu. Nimepata kwamba, hakika majaribu, yalileta uvumilivu ndani yangu, lakini kwanza yalileta uchafu mwingine mwingi juu—kama vile kiburi, uasi, kujihurumia, kulalamika, na vitu vingine vingi. Inaonekana kwamba hizi tabia zisizo za kiungu zinafaa kukabiliwa na kushughulikiwa kwa usaidizi wa Mungu kwa sababu zinazuia uvumilivu na matunda mazuri kama huruma, upendo, unyenyekevu na vitu vingine.

Biblia inazungumza kuhusu utakatifu, utakaso na dhabihu. Haya si maneno yanayopendwa; hata hivyo hivi ni vitu tunavyopitia ili kuwa kama Yesu katika tabia zetu. Matamanio ya Mungu ni kutufanya watimilifu, pasipo kukosa chochote. Anataka mwishowe tujazwe na matunda ya haki, ambayo hutuhitaji kupitia katika baadhi ya matatizo yasiyofurahisha, lakini hatimaye matatizo hayo hutusaidia kukua.

Nilinga’ng’ana na matatizo katika maisha yangu kwa muda mrefu hadi mwishowe nikajifunza kwamba Mungu atayafanyia kazi yawe mema kwa ajili yangu na kuyatumia kunisaidia kwa njia nyingi. Anataka mimi tu na wewe tujisalimishe na kusema, “Ninakuamini Mungu. Ninaamini tatizo hili litakapoisha, nitakuwa mtu bora kuliko nilivyokuwa kabla lianze!”


Haijalishi unapitia jambo gani, amini Mungu kwamba unakua na kumkaribia kila siku!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon