Mhimizane wenyewe kwa wenyewe

Mhimizane wenyewe kwa wenyewe

tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; Waebrania 10:24

 Nina marafiki watatu ambao mimi mara nyingine huenda nao kwa chakula cha mchana au kunywa kahawa. Mara nyingi tunazungumzia mambo ambayo Mungu ameweka juu ya mioyo yetu kufanya kwa wengine au mawazo ya ubunifu na njia mpya za kuwa wa baraka. Naamini majadiliano kama haya yanapendeza sana kwa Mungu.

Wazo la kuwahimiza wengine kuwa wenye nguvu katika kufanya kazi njema sio mpya. Waebrania 10:24 inasema tunapaswa kuzingatiana ili tuchochane kwa upendo na matendo mema. Tunapaswa kujifunza na kufikiri juu ya jinsi tunaweza kuwashawishi wengine kufanya kazi nzuri na matendo ya upendo, yenye manufaa.

Kumfuata Mungu peke yangu ni ngumu, lakini ninaona ni furaha zaidi nikiwa na marafiki. Ningependa kukupa changamoto ya kupata watu sawia na wewe ambao wanataka kumfuata Mungu.

Panga kuungana ili muweze kufikiri juu ya njia za vitendo za kuishi maisha ya Kikristo. Tafuta njia ambazo unaweza kumtumikia Mungu na kuuishi upendo wake pamoja.

 OMBI LA KUANZA SIKU

Roho Mtakatifu, niunganishe na marafiki wazuri ambao watanisaidia kukufuata zaidi. Ninataka kuishi maisha ya Kikristo na wengine, na kuchocheana ili kuishi katika upendo wa Mungu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon