Mungu Husikia Wanaoendelea Katika Haki

Bwana yu mbali na wasio haki; bali huisikia sala ya mwenye haki (MITHALI 15:29)

Mungu anaahidi katika andiko la leo kwamba atasikia maombi yetu tukitafuta kuwa waaminifu katika kutembea kwetu naye. Inamaanisha nini “kuendelea katika haki?” Ninafikiri njia nzuri ya kuendelea katika haki ni kuwa na msimamo.

Mtu anayekosa kuwa na msimamo ni mtu anayeonekana kukubaliana na kila ambacho watu wote wanataka kufanya, hata kama si sawa kabisa. Mtu anayekosa msimamo anajua wakati ule ambao kitu si sawa lakini anakifanya hata hivyo na kutumaini kwamba hatagunduliwa. Tunakosa msimamo tunapojua katika mioyo yetu – na hata kutokana na ushahidi wa Roho Mtakatifu- kwamba hatufai kusema au kufanya jambo fulani kisha tulifanye tu hata hivyo. Tunasema Mungu, “Mungu ananionyesha la kufanya, lakini nitafanya ninachotaka.” Katika hali kama hiyo, tunaweza tu kujilaumu sisi wenyewe tusipoona matokeo tunayotaka. Tunapokataa kukosa msimamo, na kujizatiti kuendelea katika haki kadri tuwezavyo, Mungu huona mioyo yetu, kusikia maombi yetu na kutujibu.

NENO LA MUNGU KWAKO LEO:

Ukikataa kutokuwa na msimamo, utaweka tabasamu katika uso wa Mungu.  

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon