Nia ya kubadili

Nia ya kubadili

Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako. —Kumbukumbu la Torati 30:19

Nilianza kuvuta sigara wakati nikiwa na umri wa miaka tisa. Niliipenda kwa sababu ilinisaidia, na kwa muda mrefu, sikutaka kuacha. Wakati nilipojua ni lazima niache, nilikataa kwa sababu nilifikiri ningeongeza uzito. Hicho kilikuwa kijisababu changu kwa miaka mingi. Kisha nikaingia katika mzunguko huu ambako ningeacha na kuanza tena, naacha na naanza tena.

Lakini nilifikia hatua yangu ya kuchoka wakati nilitaka kuvuta moshi sana nilianza kutoka nje wakati wa kanisa na kulala chini ya gari langu kisha nikavuta sigara. Huo ndio wakati nilijua kwamba ilibidi nifanye mabadiliko.

Mara nyingi huja hatua ya mgogoro kabla wengi wetu tuwe tayari kubadilika. Kwa mfano, wakati mwingine inachukua mshtuko wa moyo kwa mtu kuanza kuanza kula vyema. Lakini huna haja kusubiri hatua yako ya mgogoro. Unaweza tu kukata kauli na kusema, “Hiyo tosha. Nimeachana na haya. ”

Biblia inasema kwamba tunaweza kuchagua maisha. Mungu amekupa msaada na uwezo wa kubadili, lakini unapaswa kuwa tayari, la sivyo wakati wako wa mgogoro utakupiga vigumu na kwa haraka. Ni rahisi sana kuchagua maisha kabla ya kufikia hatua hiyo.

Usiogope kuwa na wasiwasi kidogo kwa muda. Hatimaye nilifikia uhuru wa kuacha kuvuta sigara, na haikuwa rahisi … lakini sikuwa nafanya hivyo peke yangu.

Ikiwa hufikiri uko tayari kubadili, nenda kwa Mungu na useme, “Nisaidie, nisaidie, nisaidie.” Habari njema ni kwamba, kwa msaada wa Mungu na uamuzi wako wa kuchagua maisha, unaweza kwa kweli, kubadilika kabisa na kuwa bora


Ombi La Kuanza Siku

Mungu, umenipa uchaguzi, na mimi nachagua maisha! Najua mabadiliko ni ngumu, lakini nakuuliza unisaidie. Kwa msaada wako na nia yangu ya kubadili, najua ninaweza kushinda kikwazo chochote.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon