
Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. MHUBIRI 3:1
Wakati kile ambacho unafanya hakikupi furaha tena—wakati ambapo hakikusisimui tena—hiyo ina maana kuwa Mungu amemaliza alichokuwa akifanya kupitia kwako. Maombi yatakusaidia kutambua iwapo Mungu anakuongoza kufanya mabadiliko.
Watu wengine hawana furaha yoyote kwa sababu wanajaribu kufanya vitu ambavyo Mungu hawaiti tena kufanya. Wanajaribu tu kuendesha farasi aliyekufa kwa kweli. Huu ndio ushauri wangu: Farasi anapoacha kwenda ndio wakati wa kushuka!
Tafuta mwelekeo wa Mungu na uwe na ujasiri wa kusema, “Nilifanya vitu kwa njia fulani kwa muda mrefu, na nilishukuru kwa kuwa na nafasi ya kuvifanya, lakini hivi sivyo ambavyo Mungu ananiongoza sasa. Ninaamini Mungu ananiongoza kufanya kitu kipya.”
Sala ya Shukrani
Baba, asante kwa kunionyesha wakati wa kufanya kitu kipya. Ninakuamini kuniongoza na kunielekeza, na ninajua kwamba furaha wakati wote huja na mpango wako. Ninakushukuru mapema kwamba utanionyesha dhahiri kabisa mwelekeo unaotaka nichukue.