Hatua 4 za kusoma neno

Hatua 4 za kusoma neno

Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu. Mithali 4:20

Watu wengi wameniuliza jinsi ya kujifunza Neno la Mungu. Hapa kuna vidokezo vinne vya manufaa:

  1. Kusudia kutenga muda. Mimi hufanya miadi na Mungu asubuhi, lakini kama hiyo haifanyi kazi kwako, pata wakati unaofanya … hata kama sio kila siku. Aanza mahali fulani na utaona matunda mazuri ambayo wakati huu huleta kwenye maisha yako!
  2. Panga maandalizi ya kujifunza Biblia. Chagua mahali unapopenda kuwa-chumba ndani ya nyumba yako ambapo unaweza kuwa peke yako.
  3. Kuwa na vifaa vyako vyote. Utahitaji Biblia yako, bila shaka, na kamusi nzuri ya Biblia, , kalamu na karatasi. Kwa njia hiyo, uko tayari kuandika maandiko yanayohusiana au kuandika kitu chini.
  4. Andaa moyo wako. Ongea na Mungu kuhusu mambo ambayo unahitaji kukiri, na kuingia wakati wako wa kujifunza kwa amani bila kitu chochote kinachoweza kukuzuia kupokea ufunuo kutoka kwa Neno la Mungu.

Tenga muda wa kujifunza Neno kwa sababu lina uwezo wa kubadilisha maisha yako na kuwa mtu ambaye Mungu anataka uwe.

OMBI LA KUANZA SIKU

Bwana, nina nia moyoni mwangu kuweka muda wa kujifunza Neno lako. Nifundishe jinsi ya kuelewa, kuridhishwa na kuruhusu kweli yako katika maisha yangu kila siku

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon