Kubali wakati wa Mungu

Kubali wakati wa Mungu

Hakuwaongoza kwa njia ya nchi ya Wafilisti, ijapokuwa ilikuwa ni ya karibu; maana Mungu alisema, Wasije wakaghairi watu hawa hapo watakapokutana na vita, na kurudi Misri; lakini Mungu akawazungusha hao watu kwa njia ya bara kando ya Bahari ya Shamu. Kutoka 2:17-18

Mungu anatupa matumaini na ndoto kwa mambo fulani ya kutokea katika maisha yetu, lakini Yeye haruhusu daima tuone wakati halisi wa mpango Wake. Ingawa haipendezi, kutokujua muda halisi mara nyingi hutuweka katika mpango wake. Tunapokubali wakati wa Mungu, tunaweza kujifunza kuishi katika tumaini na kufurahia maisha yetu wakati Mungu anafanya kazi kwenye hali zetu. Kutoka 12: 17-18 inatuambia kwamba Mungu aliwaongoza Waisraeli kwa njia mrefu, na ngumu kwenye safari yao kwenda Nchi ya Ahadi kwa sababu alijua kuwa bado hakuwa tayari kuingia. Ilikuwa wakati wa mafunzo yao, na walihitaji kupitia baadhi ya hali kubwa sana. Na katika mchakato huo, Mungu hakuwahi acha kuwatunza na kuwaonyesha kile alichotaka wafanye.

Vile vile ni kweli katika maisha yetu … Kipindi cha mafunzo ya Mungu kinatuhitaji tu tufanye kile anachotuambia kufanya wakati anatuambia kufanya hivyo, bila kuhoji au kujaribu kuhesabu kila kitu. Haijalishi mambo yatachukua muda gani, tunaweza kuwa na ujasiri daima kuwa itakuwa bora wakati tunakubali muda wa Mungu.

 OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, mimi nakubali muda wako. Siwezi kuelewa daima, lakini najua njia zako ni kamili na ninakuamini kabisa.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon