Jichoche wewe mwenyewe

Jichoche wewe mwenyewe

Kwa sababu hiyo nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu. 2 Timotheo 1:6

Upendo wa Mungu hauna masharti na ni wa milele. Nakumbuka jinsi nilishangaa na kusisimuka wakati alifunua upendo wake kwangu. Nilihisi kama ningeweza kupasuka!

Lakini baada ya muda fulani, nilipata uzoefu kwamba Mungu ananipenda, na sikusisimuka kama awali. Je! Hilo limekutokea? Je! Unaipata sasa?

Ikiwa ndivyo, naamini kuna kitu ambacho unaweza kufanya kuhusu hilo. Paulo alimwambia Timotheo kujichocha, kushawishia moto na kuimarisha moto aliokuwa nao awali. Ujumbe wa Paulo kwa Timotheo ni ujumbe wa Mungu kwako leo: Jichocheni! Acha maisha ya kuishi ukiwa umechoka na “maisha ya kale , yale yale tu.”

Tunahitaji kukumbuka hili: Tunafanya uamuzi wa kufikia maisha kwa shauku kabla ya kuwa hisia. Kwa hiyo fanya uamuzi leo kuamka kila asubuhi na msisimko kuhusu uhusiano ulio nao na Muumba wako. Jichoche mwenyewe na ustawi naye!

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, nataka daima kushangazwa na Wewe! Sitaki kuishi bila shauku. Kukujua Wewe ni jambo la ajabu, na ninachagua sasa kuishi na shauku kuhusu uhusiano wangu na Wewe

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon