Jinsi ya Kuomba bila Kukoma

Jinsi ya Kuomba bila Kukoma

Ombeni wakati wote (katika kila hali na msimu) katika Roho kwa maombi ya (kila namna) na rai. Kufikia hapo, muwe macho, mkitazama kwa kusudi lenye nguvu na uvumilivu, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote (watu wa Mungu waliotakaswa). —Waefeso 6:18

Waaminio wengi wanaelewa sana tafsiri ya Biblia ya King James ya 1 Wathesalonike 5:17. Inasema, “Ombeni bila kukoma.”

Nilikuwa nikishangaa, Bwana, nitafika vipi mahali ambapo nitaweza kuomba bila kukoma? Kwangu mimi, kifungu “bila kukoma” kilimaanisha kuendelea bila kuacha kamwe. Sikuona vile hilo lingewezekana. Sasa ninaelewa vizuri zaidi kile Paulo alimaanisha.

Alimaanisha kwamba maombi yanafaa kuwa kama kupumua, kitu tunachofanya mfululizo lakini bila ufahamu. Miili yetu inahitaji kupumua. Vilevile maisha yetu ya kiroho yameundwa kwa njia ambayo lazima yakuzwe na kudumishwa kwa maombi yasiyokoma.

Tatizo ni kwamba, kwa sababu ya mawazo yaliyofungika katika sheria na dini, tuna wazo la kupotosha kwamba tusipozingatia mpango fulani wa maombi, tunaondoka kwenye njia. Tunapokuwa na “udini” sana kuhusu maombi, kwa kufikiria kwamba lazima tuombe kwa muda fulani kwa kuwa hivyo ndivyo mtu mwingine anavyofanya, tutajiletea hukumu wenyewe. Funzo muhimu kuhusu maombi sio mkao wa mwili au wakati au mahali, lakini kujifunza kuomba kwa namna yako siku nzima. Omba kwa imani wakati wote, mahali pote.


Ni Roho Mtakatifu atakayekuongoza katika maisha ya uzoefu wa maombi.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon