kumtumaini katika mchakato

kumtumaini katika mchakato

Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. Zaburi 23:4

Mara nyingi tunafikiria kumtegemea Mungu kwa vitu tunavyohitaji au tunataka, lakini uhusiano wa kweli wa kumwamini Mungu unapita kumwamini Yeye ili kupata tu vitu. Tunahitaji kujifunza kumtumaini kupitia mchakato wa kufikia mambo hayo tunayotaka.

Kulikuwa na wakati katika maisha yangu wakati nilizingatia sana kumtegemea Mungu kwa vitu, nikisema, “Ninataka hii, Mungu,” na “Ninahitaji hiki na kile, Mungu.” Alianza kunionyesha kuwa kupata vitu vyote hakukuwa suala muhimu zaidi katika maisha yangu.

Alitaka kunifundisha jinsi ya kumwamini Yeye kiasi cha kutembea kupitia hali kwa utulivu na mtazamo mzuri kwa msingi thabiti. Alihitaji mimi kujifunza kwamba Yeye hawezi kutuokoa kila wakati tunapotaka atutoe katika hali fulani, lakini Yeye huwa pamoja nasi wakati tunapopitia hali hiyo.

Mungu hatatuokoa daima kutoka kila kitu tunapofikiri anapaswa, lakini Yeye daima amekuwa nasi. Leo, badala ya kutazamia tu matokeo ya mwisho, tambua kuwa Mungu yuko pamoja nawe sasa. Yeye yuko karibu nawe, basi mwamini Yeye kutembea nawe katika hiyo hali.

 OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, ninafurahi sana kwamba uko pamoja nami sasa. Siamini tu Wewe kunipa mambo, lakini ninakuamini kupitia hali ya kila siku ya maisha

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon