Kubebwa katika Mikono Yake

Kubebwa katika Mikono Yake

Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini! ZABURI 91:2

Kwenye hatua mbalimbali za maisha yetu, sisi wote huhisi “tunaondoka kwenye kina cha maji ya urefu wetu” au “tuko ndani ya kina cha maji yaliyo juu ya vichwa vyetu.” Kuna shida pande zote: tunapoteza kazi, mtu anafariki, ugomvi katika familia, au ripoti mbaya inatoka kwa daktari. Mambo haya yanapofanyika, tunashikwa na hofu kwa sababu tunahisi tumepoteza udhibiti.

Lakini fikiria hili: Ukweli ni kwamba hatujawahi kudhibiti vipengele muhimu maishani. Kitu pekee kinachotushikilia—na kitu ambacho tunaweza kushukuru sana kwacho—ni neema ya Mungu, Baba yetu, na hiyo haitawahi kubadilika. Mungu hajawahi kuwa nje ya kina chake cha urefu, na kwa hivyo tuko salama tunapokuwa katika “kina cha kirefu” cha maisha kwa sababu tunaweza kuamini kwamba atatubeba katika miono yake wakati wote.


Sala ya Shukrani

Asante, Baba, kwamba wewe ni ngome kwangu. Ninajua kwamba kwa sababu uko nami, ninaweza kuhisi usalama na ulinzi. Asante kwamba licha ya vile maisha yanavyoweza kuwa magumu, ninaweza kuwa na amani kwa sababu hutawahi kuniachilia.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon