Dumu katika upendo wake

Dumu katika upendo wake

Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake 1 Yohana 4:16

1 Yohana 4:16 inasisitiza kwamba tunahitaji kuwa na ufahamu wa upendo Mungu alionao kwetu. Ni rahisi kwetu kusema “Mungu anipenda” bila kuelewa kweli tunachosema. Ufahamu wa upendo wake haupaswi kuwa tu ukweli wa kibiblia kwamba tunaelewa katika akili zetu lakini ukweli halisi katika maisha yetu.

Aya hii inasema, Mungu ni upendo, na yeye anayeishi na anaendelea katika upendo anakaa na anaendelea katika Mungu, na Mungu anakaa na anaendelea ndani yake.

Neno hili katika mstari huu inamaanisha “kukaa, kuishi ndani.” Haina maana ya kutembelea tu; inahusu kukaa au kubaki.

Upendo wa Mungu sio ukweli tu wa kukariri au hisia za kudumu. Upendo wake uko hapa kukaa. Haupo tu katika nyakati nzuri na kutuacha wakati mambo ni mabaya; Upendo wa Mungu daima unabaki, hivyo tunapaswa kubaki katika upendo Wake.

Kila mmoja wetu anaweza kuvuna mavuno makubwa ya ukomavu wa kikristo tunapoegemea upendo wa Mungu. Utakomaa katika nyakati ngumu unapokaa katika upendo wa ajabu Mungu anao kwako.

OMBI LA KUANZA SIKU

Bwana, ninajitahidi leo kuishi katika upendo ulio nao kwa ajili yangu. Mambo mengi yanabadilika, lakini upendo wako haubadiliki kamwe, kwa hiyo naamua kukita mizizi katika upendo wako wa ajabu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon