
Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo, naye amesulibiwa. 1 Wakorintho 2:2
Wakristo wengi wanateseka kwa sababu wanashughulika sana kutafuta ujuzi wa kimwili badala ya Neno la Mungu. Bwana mwenyewe alisema, Watu wangu wameangamia kwa kukosa ujuzi … (Hosea 4: 6).
Paulo alikuwa mwanafunzi mwenye elimu ya kimwili. Alijiona kuwa bora zaidi kuliko wengine na hata alitaka kuua Wakristo. Cha kushangaza, Mungu alikuwa na mipango mingine kwa ajili yake na kujidhihirisha kwa Paulo kwa njia iliyobadilisha maisha yake milele.
Wakati Paulo alitambua kwamba kutafuta ujuzi wa kimwili hakulinganishwi na umuhimu wa ujuzi wa kiroho, aliamua kufuata tu hiyo badala yake. Kama Paulo, tunahitaji kutambua umuhimu wa kujifunza mambo ya kiroho.
Badala ya kutafuta vitu vya kidunia na kujaza vichwa vyetu kwa vitu ambavyo havijalishi, tunapaswa kusoma, kujifunza, kutafakari na kujaza akili zetu kwa Neno la Mungu.
Naweza kukuambia kutokana na uzoefu kwamba kujua Neno la Mungu kutabadilisha maisha yako. Kulimbadilisha Paulo kuwa mmoja wa Wakristo wakuu ambao waliwahi kuishi, na inaweza kukugeuza na kukuongoza katika hatima yako ya kushangaza katika Kristo.
Ninakuhimiza leo kutafuta ujuzi wa kiroho unaopatikana katika Neno la Mungu. Wingi wa Neno la Mungu katika moyo wako na akili yako itakusaidia kupata kile unachotafuta
OMBI LA KUANZA SIKU
Bwana, sitaki kupoteza muda wangu na ujuzi wa kimwili ambao haujalishi. Kama Paulo, nisaidie kufuata zaidi ya chochote kingine ujuzi wa kiroho unaopatikana katika kukujua na kujua Neno lako.