Uvumilivu hulipa

Uvumilivu hulipa

Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele. Mathayo 19:29

Katika miaka ya mwanzo tulipokuwa tukijenga huduma yetu, Dave na mimi tulipitia vipimo vingi vya kujaribiwa. Nilihitaji kufanya kazi juu ya mtazamo wangu. Tulihitaji kufanya kazi kwenye ndoa yetu na jinsi tulivyotumia fedha.

Kwa miaka sita nilinunua soksi na chupi zangu katika mauzo ya karakana. Tulingángána kabisa-na nilikuwa nikifundisha juu ya utoaji wa Mungu katika maisha yetu!

Siyo hayo tu, haikuwa maarufu kwa wanawake kuhubiri wakati huo. Tulipoteza marafiki na tulikuwa na watu wa jamii yetu ambao hawakutaka chochote na sisi. Ilikuwa vigumu, na wakati mwingine nilitaka kuacha.

Lakini leo nimefurahi sana kwamba nilishikamana na Mungu kwa sababu kuna watu ulimwenguni pote ambao wamesaidiwa kwa sababu ya kile ambacho Mungu amefanya kupitia huduma yetu.

Maandiko yanatuambia katika Mathayo 19 kwamba tutatakiwa kuacha mambo “muhimu” nyuma ili kumfuata. Hatukuwa na kila kitu ambacho tulidhani tulihitaji wakati huo, lakini kuachana na hayo yote ilikuwa ya thamani kubwa.

Endelea katika kutembea na Mungu, hata wakati ni ngumu. Endelea kumtazamia, na utaona manufaa yake wakati unapoona ushindi alionao kwako.

 OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, wakati mwingine ni vigumu kustahimili katika maisha ya Kikristo, lakini najua kwamba uvumilivu utalipa mwishowe. Asante kwa kunipa nguvu ninazohitaji kuendelea. Mimi nitakufuata Wewe pekee, kwa sababu Wewe ndio mambo yote.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon