Kuishi Huru Kutokana na Majuto

Kuishi Huru Kutokana na Majuto

Ila natenda moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele… WAFILIPI 3:13

Bila usaidizi wa Mungu, tuna matatizo ya kufanya vitu kwa kiasi. Tunaweza kula kupindukia, tunaweza kutumia pesa nyingi, kuburudika sana, na kuongea sana. Sisi hukiuka mipaka katika lolote tunalotenda kwa sababu tunaongozwa na hisia zetu. Tukihisi kufanya kitu, tunakifanya bila kufikiri kuhusu matokeo. Baada ya kukifanya kitu hicho na hakiwezi kurekebishwa, tunaanza kujuta kukifanya.

Lakini shukuru kuwa hatuhitaji kuishi tukijuta. Mungu hutupatia Roho wake ili kutuwezesha kufanya uamuzi sahihi na wenye hekima. Hutusihi, kutuelekeza na kutuongoza, lakini bado uamuzi uko juu yetu. Ili kuunda desturi mpya, utahitajika kufanya uamuzi kuwa hutafanya kile unachohisi kufanya isipokuwa kama kinakubaliana na mapenzi ya Mungu. Kwa usaidizi wa Roho Mtakatifu, unaweza kubadilisha matendo yako na kuishi maisha yaliyo huru kutokana na majuto!


Sala ya Shukrani

Ninakushukuru, Baba, kwamba, silazimiki kuishi nikiwa nimekwama katika majuto kwa sababu ya makosa yangu. Umenisamehe na kunitengenezea njia mpya. Nisaidie kusahau makosa yangu ya jana na kufanya uamuzi bora leo. Nisaidie kuishi huru kutokana na majuto dhidi ya mambo yaliyopita na kuwa mwenye imani tele kwa ajili ya mustakabali wangu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon