Hatimaye, ndugu zangu, mambo yoyote yaliyo ya kweli yoyote yaliyo ya staha, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote yenye kupendeza, yoyote yenye sifa njema; ukiwapo wema wowote, ikiwapo sifa nzuri yoyote, yatafakarini hayo. WAFILIPI 4:8
Tukitafakari juu ya vitu ambavyo vimeenda kombo katika maisha yetu, inaweza kuanza kuonekana kwamba hakuna liendalo vizuri, lakini hilo si kweli. Huenda umekuwa na matatizo mengi katika maisha yako, lakini nia ya shukrani hutambua kuwa nyakati nzuri kuliko nyakati mbaya katika maisha yako.
Tazama maisha yako kikamilifu badala ya kutafakari kuhusu mikasa tu, majaribu na masikitiko. Kutafakari mazuri hukupa ujasiri wa kukabiliana na mabaya na kuepuka kuishi katika hofu. Kutambua kwamba Mungu yuko nawe, akikusaidia njiani, hukupa ujasiri unaohitaji ili kukabili mustakabali kwa ujasiri, ukijua kwamba kwa kweli unaweza kushinda kizuizi chochote katika nguvu na uwezo wa Bwana.
Sala ya Shukrani
Baba, ninapohisi kukata tamaa, nisaidie kuona vitu vyote vizuri ulivyonifanyia. Ninakushukuru kwamba mazuri ni mengi kuliko mabaya. Na ninakushukuru kuwa kuna mambo mengi mazuri yanayokuja.