Kuwa na Wazo la Mungu Ananipenda

Kuwa na Wazo la Mungu Ananipenda

Wapenzi na mpendane kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. — 1 YOHANA 4:7

Kadri tunavyotafakari kuhusu upendo wa Mungu juu yetu usio na masharti, ndivyo tunaanza kuwa na tajriba nao. Ninakuhimiza kujizoesha kutambua na kujua upendo wa Mungu juu yako. Paulo aliomba katika Waefeso 3 kwamba watu watapata kufahamu upendo wa Mungu kwao wao wenyewe. Hayo ndiyo maisha Mungu anataka tuishi—maisha ambayo kwa kweli tunajua na kuwa na upendo wake usiokoma, usio na masharti.

Nilikuja kutambua upendo wa Mungu juu yangu kupitia kwa kujifunza maandiko kuhusu upendo wake. Niliyatafakari na kuyakiri kutoka kwenye kinywa changu. Nilifanya hivi mara nyingi kwa muda wa miezi mingi, na wakati wote ufunuo wa upendo wake usio na masharti ukaanza kuwa wa kweli kwangu. Kitu hicho hicho kinaweza kufanyika kwako. Iwapo utasoma Neno la Mungu, ukisimama kwenye kila ahadi ya upendo wa Baba, utajifunza kuishi katika ufunuo unaobadilisha kwamba unapendwa. Lifikirie hivi: Hakuna dakika moja katika maisha yako ambayo hupendwi.


Unapendwa!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon