Maneno Unayosema

Maneno Unayosema

Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; na wao waupendao watakula matunda yake. —Mithali 18:21

Mtume Petro anatuambia wazi kwamba kufurahia maisha na kuona siku njema, na kuwa na fikra chanya na mdomo, zinahusiana. Tukibadilisha maneno yetu, tunaweza kubadilisha maisha yetu!

Mdomo wetu husema kilicho mawazoni mwetu, kuhisi na kutaka. Nia zetu hutuambia cha kufikiria, na sio lazima kiwe kile Mungu anafikiri. Nia zetu hutuambia kile tunataka, sio kile Mungu anataka. Hisia zetu hutuambia kile tunahisi, sio kile Mungu anahisi. Nafsi yetu inapozidi kusafishwa, inafundishwa kuwa na fikra za Mungu, matamanio, na hisia; halafu tutaanza kuzungumza uzima badala ya mauti.
Maneno yako, kama kiakisi cha fikra zako, yana nguvu za kuleta baraka au uharibifu, sio tu kwa maisha yako bali kwa maisha ya watu wengine wengi. Katika 1 Wakorintho 2:16, Neno la Mungu linatufundisha kwamba tuna nia ya Yesu na kwamba tumeshikilia fikra, hisia na makusudio za moyo wake.

Hatuyadhihirishi kila wakati, lakini tunakua kila siku na kubadilishwa kuwa mfano wa Kristo. Yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu (Wafilipi 1:6). Kadri tunavyomkaribia Mungu, ndivyo tutakavyopata ushindi juu ya nia, mdomo, hali na fikra mbaya.


Hata kama utaenda mbali kiasi gani, ninajua unaweza kubadilika kwa sababu nilibadilika. Ilichukua muda na usaidizi wa Roho Mtakatifu, lakini ilifaa.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon