Maombi ya Shukrani

Maombi ya Shukrani

Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu. —1 WATHESALONIKE 5:18

Baada ya kutuagiza kuomba bila kukoma katika 1 Wathesalonike 5:17, Mtume Paulo anatumia msitari wa 18 akituelekeza kumshukuru Mungu kwa kila kitu, bila kujali vile hali zetu zilivyo, akieleza kwamba haya ni mapenzi ya Mungu juu yetu.

Kama tu vile maombi yalivyo mtindo wa maisha unaotuleta karibu na Mungu, shukrani ni vivyo hivyo. Kumpa Mungu shukrani sio kitu tunachofanya mara moja kwa siku tukiwa tumekaa mahali fulani na kuanza kufikiria kuhusu mambo yote mazuri ambayo ametutendea na kusema tu, “Asante Bwana.” Si kitu tunachofanya tu wakati wa kula. Huo unaweza kuwa udini mtupu, kitu tunachofanya tu kwa sababu tunafikiria kwamba Mungu anakihitaji.

Shukrani za kweli hutiririka bila kukoma kutoka kwa moyo uliyo na wingi wa shukrani na sifa kwa Mungu kwa jinsi alivyo na yale anayoyafanya. Si kitu kinachofanywa kutimiza masharti, kupata kibali, kupata ushindi au kustahili kupata baraka.

Aina ya shukrani ambayo Mungu Baba anatamani ni ya kutoka moyoni na hutiririka kutoka kwetu mara nyingi kwa sababu tunaendelea kuona na kutambua vile Mungu alivyo mwema kwetu kila wakati. Acha tuwe wenye shukrani na tuseme hivyo!


Kuwa mwingi wa shukrani kila mara, kwa kutambua bila kukoma, kukiri, na kutukuza jina lake katika maombi ya sifa na ibada.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon