Mwepesi wa Kusamehe

Mwepesi wa Kusamehe

Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi. —WAEFESO 4:32

Biblia inatufundisha kuwa “tayari na huru” kusamehe. Hicho ni kiwango cha Mungu kwetu sisi, haijalishi tunavyohisi kukihusu. Tunafaa kuwa wepesi wa kusamehe.

Kulingana na 1Petro 5:5, tunaweza kujivisha sifa za tabia ya Yesu Kristo, kumaanisha kwamba, tunaweza kuchagua kuwa wavumilivu kwa muda mrefu, wenye subira, wasio kwazika kwa urahisi, wasio kasirika haraka, wepesi wa kusamehe, na wenye kujawa na huruma. Ufafanuzi wangu wa “huruma” ni kupuuza ninayofanyiwa ambayo yanadhuru na kugundua sababu ya kufanywa. Mara nyingi watu hufanya mambo ambayo hata wao wenyewe hawayaelewi, lakini wakati wote huwa kuna sababu ya watu kufanya wanavyofanya. Pengine huwa wanadhurika na katika uchungu wao huenda wasigundue kwamba wanadhuru mtu mwingine.

Mungu husamehe! Lazima tuwe wenye huruma na kusamehe, vile tu Mungu ndani ya Kristo hutusamehe makosa yetu. Huwa haoni tu kuwa tunachofanya ni makosa, lakini pia huelewa kwa nini tulikifanya, na ni mwenye huruma na huvumilia kwa muda mrefu. Chaguo la kusamehe ni letu. Mungu hawezi kulazimisha mtu kusamehe. Hata kama huelewi, amini kwamba njia ya Mungu ndiyo nzuri kabisa. Inafanya kazi. Anaweza kuchukua kile Shetani alikusudia kuharibu na kukibadilisha kuwa chema kwa ajili yako.


Tunaweza kusamehe ili kumzuia shetani kututumia kwa manufaa yake.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon