
Na Wewe, Bwana, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu na mwinua kichwa changu. Zaburi 3:3
Mungu ana mipango mema kwako na anataka ufurahie maisha yako. Hataki uishi na roho ya uzito, kukata tamaa, unyogovu au kudhoofika. Habari njema ni, mawazo yako na mtazamo wako unaweza kubadilika wakati unapomtazama Mungu na kumruhusu kukuinua.
Mtunga-zaburi alisema kuwa Mungu ni ngao kwa ajili yangu, utukufu wangu, na mwinua kichwa changu. Fikiria juu ya maneno hayo “mwinua kichwa changu.” Mtu anapokuwa anazunguka na kichwa chake kimeegemea chini, tutadhani wanasikitika au wana huzuni. Ikiwa ndivyo unavyohisi, jua leo kwamba Mungu anaweza kuinua kichwa chako na roho zako.
Kumbuka, Mungu ana mpango mzuri na baadaye na tumaini kwa kila mmoja wetu. Kwa kuwa Yeye yu pamoja nasi, tunaweza kufikiri na kuzungumza kwa makubaliano na mapenzi yake. Tunaweza kufanya mazoea kuwa chanya katika kila hali inayojitokeza. Na wakati hali zetu ni ngumu na zenye changamoto, tunaweza kutarajia Mungu kutuletea mema kama alivyoahidi katika Neno Lake.
OMBI LA KUANZA SIKU
Mungu, Wewe ndio utukufu wangu na mwinua kichwa changu. Ninachagua kukuangalia Wewe. Nisaidie kuweka mtazamo wangu juu yako na nikuamini wewe kuleta mipango yako mizuri kupita katika maisha yangu leo.