Moyo mkamilifu

Moyo mkamilifu

Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake. 2 Mambo ya Nyakati 16:9

Muda na wakati tena katika maisha yangu, Bwana amenikumbusha kwamba Yeye hatafuti utendaji kamili kutoka kwetu, lakini mioyo kamilifu. Watu wengi wanafikiri Mungu hatawatumia mpaka kila eneo la maisha yao likamilike. Aina hii ya kufikiri inawazuia watu kuruhusu Mungu kuwatumia. Lakini Mungu anatutumia licha ya yote, si kwa sababu ya chochote.
Wakati mwingine watu “hutupenda” kulingana na utendaji wetu. Ikiwa unafanya kile wanataka ufanye, wanakukubali; lakini kama hutendi, wanakukataa. Upendo wa Mungu unamtegemea tu Mungu. Anakupenda na kukukubali jinsi ulivyo.
Hii haina maana tunapaswa kuwa na mtazamo usio sawa na tusitamani kuishi maisha takatifu. Mtu ambaye moyo wake ni mkamilifu kwa Mungu daima anatamani kwa bidii na kwa shauku kumpendeza Mungu katika vitu vyote, lakini anaelewa kwamba Mungu hatamkataa kamwe kwa sababu ya udhaifu wake au makosa yake.
Anataka kutupenda na kutusaidia wakati tuko dhaifu. Hebu Mungu akupende, na kwa upande wako, mpe upendo wako kwa moyo mkamilifu!

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, najua kwamba unanipenda licha ya udhaifu wangu na makosa yangu. Ninakushukuru kwa upendo huu na ninakupa moyo wangu, najua kwamba unaweza kunitumia wakati ninakufuata kwa moyo mkamilifu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon