
Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. WARUMI 5:8
Mungu anatutaka tuhakikishiwe upendo wake na tusiruhusu kitu chochote kututenganisha nao. Kwa moyo uliojaa shukrani, tunaweza kutulia tukijua kwamba Mungu anatupenda katika nyakati nzuri, na anatupenda katika nyakati ngumu. Mungu anatupenda siku ambazo tumetenda mema na siku ambazo hatujatenda mazuri. Shukuru kwamba upendo wa Mungu hauna masharti.
Anatupenda, sio kwa misingi ya kile tunachofanya, lakini kwa wale tumekuwa ndani ya Kristo. Kwa maneno mengine, tunahitaji kujua kwamba sisi ni wana wapendwa wa Mungu, na kujua jinsi ya kutenganisha “Nani” yetu kutoka kwa “Tenda” yetu. Hatuwezi kufanya kila kitu inavyostahili kila wakati, lakini bado tuna haki mbele ya Mungu kupitia kwa Kristo. Mungu bado anatupenda kila wakati wa kila siku. Hicho ni kitu cha kusherehekea!
Sala ya Shukrani
Baba, ninashukuru kwamba upendo wako juu yangu una misingi yake ndani ya niliye katika Kristo, sio katika kile ninachofanya kila siku. Hata ingawa ninataka kukupendeza kwa matendo yangu, ninakushukuru kwamba upendo wako juu yangu ni wa kina kirefu kuliko hilo. Unanipenda kama mwana wako na hakuna kinachoweza kuondoa upendo wako.